Posts

Katibu Mkuu Chadema Ahojiwa Kuhusu ‘Watu Wasiojulikana’

Image
Dk Vincent Mashinji. KATIBU Mkuu wa Chadema , Dk Vincent Mashinji amesema polisi wamemhoji wakitaka kujua kuhusu kauli zake za watu wasiojulikana kama anaweza kuwatambua. “Watu wasiojulikana ambao tulikuwa tunawaongelea ni kwamba, imezoeleka kwa polisi kunapokuwa na tukio kubwa wanasema watu wasiojulikana, kwa hiyo lengo langu lilikuwa ni kuita wananchi  kurudi kwenye Polisi Jamii ili kuondokana na hili la watu wasiojulikana,” alisema Dk Mashinji. Katibu mkuu huyo wa Chadema, leo Jumatatu ameamua kwenda kuripoti Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini hapa. Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Chadema, Tumaini Makene ilisema Dk Mashinji aliambatana na wasaidizi wake kutoka makao makuu ya chama hicho. “Katibu mkuu amewasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam, kuitikia wito wa Polisi uliotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, kuwa anatakiwa kufika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (

Breaking News: Watu Wasiojulikana Wavamia Ofisi za Wakili wa Manji

Image
Polisi wakiwa eneo la tukio. Ofisi ya mawakili ya Prime Attorneys imevamiwa usiku wa manane na watu wasiojulikana ambao wameiba kasiki lenye fedha na nyaraka. Mmoja wa mawakili katika ofisi hiyo,  Hudson Ndusyepo amesema ofisi yao imevunjwa na tayari ameenda polisi kutoa taarifa. Ndusyepo ambaye ni miongoni mwa mawakili wanaomtetea mfanyabiashara maarufu Yusuf Manji katika kesi ya uhujumu uchumi, amesema kabla ya wizi huo, waliohusika walimfunga mlinzi kwa kamba.   Milango ilivyovunjwa. Kampuni ya Prime Attorneys katika tovuti yake inaeleza ilianzishwa mwaka 2010. Ofisi za kampuni hiyo zipo Jengo la Prime House lililopo Mtaa wa Tambaza, Upanga jijini Dar es Salaam. Ofisi hizo zipo kwenye jengo la ghorofa tano lililopo jirani na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wilayani Ilala. Leo Asubuhi barabara ya kuingia eneo hilo ilifungwa kwa muda na polisi ambao walitumia magari yao kuziba njia na kuweka uzio wa  utepe wa rangi ya njano. Wakili

Vyakula Vinavyoliwa na Mgonjwa wa Vidonda Vya Tumbo

Image
LEO tutaangazia vyakula tiba kwa wagonjwa wa vidonda vya tumbo. Tutaangalia aina ya vyakula anavyopaswa kula au kuviepuka mgonjwa wa vidonda vya tumbo (Ulcers) ili kupata nafuu na kuishi bila kusumbuliwa nao. Ili kupunguza makali au kujiepusha kabisa na ugonjwa huo unapaswa kujiepusha kula vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi. Epuka ulaji wa vyakula vilivyopikwa na kuungwa viungo vingi vya aina mbalimbali, kama vile pilipili kali za aina zote na viungo vingine vyenye ladha ya ukali ambavyo hutiwa ndani ya mboga ama chakula ili kuongeza ladha. Pombe na kahawa au vinywaji vingine vyenye caffeine, vinaweza kuleta matatizo kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo na kwa mtu asiye navyo anaweza kupatwa na tatizo, hivyo ni vyema kuepuka au kutumia kwa kiasi kidogo vinywaji hivyo kwani huongeza asidi tumboni na hivyo vinaweza kusababisha vidonda au kuzidisha maumivu kwa anayeumwa. Kuna uhusiano kati ya ulaji chumvi na vidonda vya tumbo. Mgonjwa anashauriwa kuepuka ulaji wa

Je unajua vyoo vya kukaa vina madhara kiafya kwa watumiaji

Image
Nyumba haiwezi kuwa kamili bila kuwa na huduma hiyo ya choo, Hata hivyo, pamoja na umuhimu wa choo, lakini si kila nyumba iliyo na choo au hata zile ambazo zina huduma hiyo, basi vyoo ni vibovu, havina hadhi. Zipo aina mbalimbali za vyoo kwa matumizi ya binadamu katika maisha yake ya kawaida. Vyoo vina matumizi mengi ingawa  bado  watu wengi  hasa katika nchi maskini na zinazoendelea ikiwamo Afrika wanatumia choo cha kuchuchumaa wakati wa kujisaidia, lakini mijini na katika nchi zilizoendelea, wao hutumia vyoo vya kukaa. Nyumba nyingi mijini na ofisi mbalimbali zinazojengwa hivi sasa, huwekewa vyoo vya kukaa. Hata zile za zamani zinakarabatiwa na kubadilishwa kwa kuwekewa hivi ambavyo vinaonekana vya ‘kisasa’. Mgunduzi wa vyoo vya aina hii, Thomas Crapper anasema kwa mtazamo wake aliona kukaa wakati wa kujisaidia ni utambulisho wa ustaarabu na maendeleo. Hata hivyo, madaktari wanapingana naye wakisema kujisaidia katika vyoo vya kukaa kuna madhara kiafya kwa k

ANGALIA PICHA YA KWANZA MADAKTARI WALIOKOA MAISHA YA TUNDU LISSU

Image
                       Timu ya Madaktari waliookoa uhai wa Mh Lissu kwa huduma ya dharula Mjini Dodoma wakiwa chini ya Dr. Mpoki(Katibu Mkuu W/Afya), Dr. Mponda (Orthopaedic), Dr. Samwel (Orthopaedic),na Dr. frank.Mh Lissu tayari ameondoka katika ardhi ya Tanzania na kwenda Nairobi Kenya kwa matibabu zaidi akiambatana na mkewe kipenzi wakili msomi Alicia Lissu sambamba na Mwenyekiti wa Chadema Mh. Freeman Mbowe, na Mh. Peter Misigwa.

Kanisa la Askofu Gwajima labomolewa

Image
Dar es Salaam. Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo Mbezi Inn linalomilikiwa na Askofu Josephat Gwajima limebomolewa. Nyumba hiyo ya ibada ambayo pia ilikuwa ikitumika kama kituo cha maombezi imebomolewa na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads). Imeelezwa kanisa hilo limejengwa ndani ya hifadhi ya Barabara ya Morogoro ya mita 121.5. Kwa mujibu wa waumini wa kanisa hilo, pia limekuwa likitumika  kama kituo cha kufundishia wachungaji limebomolewa jana jioni hali iliyosababisha waumini wa Kanisa hilo kusalia nje. Mwananchi imefika katika kanisa hilo na kukuta  vitu vikiwa nje na baadhi ya waumini wakiendelea  na maombi nje. Mmoja wa waumini ambaye hakutaka kujitambulisha kwa madai si msemaji, amesema kanisa leo limebomolewa lakini injili inaendelea kuhubiriwa kama kawaida . "Tunaendelea na huduma na kesho tutakuwa na ibada itakayoanza saa kumi jioni "amesema. Muumini mwingine pia amesema hali ilikuwa mbaya jana wakati kanisa hilo linabomolewa kwani wali

Kauli ya Rais Magufuli Baada ya Kupata Taarifa za Lissu

Image
RAIS John Magufuli ameeleza kusikitishwa kwake kutokana na kushambuliwa kwa kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema). “Nimepokea kwa masikitiko tukio la kupigwa risasi Mh.Tundu Lissu, namuombea kwa Mwenyezi Mungu aweze kupona haraka. Aidha, vyombo vya dola viwasake wale wote waliohusika na tukio hili la kinyama na kuwafikisha ktk mikono ya sheria,” amesema Rais Magufuli. Stori zinazo husiana na ulizosoma

BREAKING: Tundu Lissu Apigwa Risasi

Image
MBUNGE wa Singida Mashariki, Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu amevamiwa na watu wasiojulikana kisha kumpiga risasi zinazodaiwa kuwa tano. Tukio hilo linadaiwa kutokea leo akiwa nyumbani kwake Area D Mjini Dodoma ambapo watu hao walimvamia akiwa kwenye gari kisha kumpiga risasi za miguuni na tumboni. Imeelezwa kuwa alikuwa akitokea Bungeni na alienda Nyumbani kula chakula cha mchana.  Dereva wake akiwa ameshika nguo na viatu vya Tundu Lissu Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema amesema kuwa Mh. Lissu amepigwa risasi zaidi ya mbili alipokuwa amweetoka bungeni na kwenda nyumbani kwakwe kwa ajili ya chakula cha mchana. Gari la Mbunge Lissu likionekana na baadhi ya matundu zilipopigwa Risasi  Kwa mujibu wa taarifa zilizopo ni kwamba amekimbizwa hospitali na sasa yupo chumba cha upasuaji. "Hli ya Tundu Lisu ni mbaya Sana

Kutajwa Sakata la Madini… Waziri Simbachawene, Ngonyani Wajiuzulu

Image
Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene. WAZIRI wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) , George Simbachawene na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani wameandika barua za kujiuzulu nyadhifa hizo ili kupisha uchunguzi baada ya kutajwa kuhusika kwa ubadhilifu kwenye Ripoti za Uchunguzi wa Biashara ya Madini ya Almasi na Tanzanite. Uamuzi a viongozi hao umekuja ikiwa ni dakika chache baada ya Rais Magufuli kupokea Ripoti hiyo kutoka kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambapo Rais aliwataka viongozi wote wa serikali walioko madarakani na wametajwa kuhusika kwenye kashfa hizo waachie ngazi ili kupisha uchunguzi wa vyombo vya usalama. Kwa upande wake, akiongea na Mwananchi leo Alhamisi mchana mara baada ya hafla ya makabidhianao ya ripoti hizo, Ngonyani amesema amepokea kauli ya Rais kwa mikono miwili na sasa anaandika barua ya kujiuzulu nafasi hiyo. Naibu Waziri w

Breaking News: Mtekaji Wa Watoto Arusha Auawa Kwa Kupigwa Risasi

Image
Mtuhumiwa Samson Petro enzi za uhai wake. Kijana aliyehusika na matukio ya utekaji watoto mkoani Arusha, Samson Petro (18) amefariki dunia kwa kupigwa risasi na polisi. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa kifo hicho alipozungumza na waandishi wa habari. Kamanda Mkumbo amesema kijana huyo ambaye alikamatwa mkoani Geita alikokuwa amekimbia kabla ya kurejeshwa Arusha alitaka kukimbia alipokuwa anakwenda kuwaonyesha polisi watuhumiwa wenzake wa utekaji  saa tano usiku wa jana Jumatano. Hivi karibuni alipokamatwa mkoani Geita, kijana huyo ambaye sasa ni marehemu alikiri kuwateka watoto wanne mkoani Arusha baada ya kukamatwa mjini Katoro wilayani Geita alikotekeleza tukio lingine la utekaji. Akizungumza akiwa chini ya ulinzi wa polisi wiki iliyopita, kijana huyo alisema watoto wawili aliwarudisha kwa wazazi wao baada ya kupewa Sh300,000. Alisema wengine wawili aliwatelekeza mtaani baada ya wazazi wao kutotoa kiasi cha fedha w

Hashim Rungwe Ashikiliwa na Polisi Dar

Image
Hashim Rungwe Spunda. ALIYEKUWA mgombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Hashim Rungwe Spunda anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa siku nne sasa. Rungwe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chaumma) anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam akituhumiwa kughushi nyaraka. Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema leo Septemba 5 kuwa, Rungwe anashikiliwa kituoni hapo kwa siku nne. Hata hivyo, Kamanda Mambosasa hakutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo akisema hana taarifa za kutosha.

DENTI ACHARANGA WATU VISU MTAANI!

Image
Paulo Ndensai akiuguza majeraha. MWANAFUNZI wa kidato cha pili katika shule moja ya sekondari Wilaya ya Kinondoni jijini, Samuel Wilson, Jumanne iliyopita, saa mbili usiku, alifunga mtaa maeneo ya Mwenge Mlalakuwa na kuwachoma visu watu kadhaa akiwemo Paulo Ndensai na Yasin Mohammed. Akisimulia kwa uchungu tukio hilo mmoja wa mashuhuda alisema mwanafunzi huyo alikuwa akimpiga kijana mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Mohammed huku akimchoma kwa kisu alichoshika hali iliyowafanya wananchi waliokusanyika eneo hilo kukimbia kwa kuhofia usalama wao. Shuhuda huyo alisema denti huyo akiendelea kumshambulia Mohammed ambapo chanzo cha ugomvi huo hakijawekwa bayana, kaka yake Mohammed aitwae Paulo Ndensai alitokea na kwenda kumuokoa mdogo wake. “Katika harakati za kumuokoa mdogo wake, mtuhumiwa alimuacha aliyekuwa akimshambulia na kuhamishia varangati kwa kaka mtu ambapo alimchoma kwa kisu kichwani juu kidogo ya sikio la kushoto, kingine akamchoma kichwani juu, hali

RAILA ODINGA AMWITA KIBA KENYA, ATUMIWA NDEGE BINAFSI

Image
Alikiba. DAR ES SALAAM: Upepo mwanana bado unaendelea kumpuliza, staa namba moja wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ baada ya mgombea anayewakilisha Muungano wa Vyama vya Upinzani nchini Kenya (NASA), Raila Omolo Odinga, kudaiwa kumuita nchini humo. Kwa mujibu wa chanzo kisicho na chembe ya shaka, Kiba anayesumbua kwa sasa na wimbo wake wa Seduce Me, alipata mwaliko huo mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwa ni saa chache mara baada ya Odinga kushinda kesi ya uchaguzi Katika Mahakama ya Juu aliyokuwa amemfungulia Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ambaye mambo yalimuwia mazito. Kenyatta alitangazwa mshindi wa nafasi ya urais na Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IBEC) katika uchaguzi uliofanyika nchini humo Agosti 8, mwaka huu ambapo Odinga alifungua kesi hiyo mahakamani. Baada ya mahakama kupitia hoja za pande zote, iliufuta uchaguzi huo kwa kueleza kuwa tume ya uchaguzi haikuzingatia uadilifu. ODINGA KICHEKO Mara baada ya hukumu hiyo kutolewa mahakaman

BREAKING: Wabunge wa Upinzani watoka nje ya Bunge

Image
Wabunge wa Ukawa wasusia na kutoka nje shughuli ya kuapishwa kwa wabunge wa viti maalum 7 wa CUF. Wabunge hao ni wale waliopatikana baada ya Mwenyekiti wa Chama hicho Prof Lipumba kutangaza kuwavua uanachama Wabunge 8 wa chama waliokuwepo kwasababu mbalimbali ikiwemo ya maadili.

RIPOTI YA MAKINIKIA ALMASI, TANZANITE BUNGENI KESHO

Image
             WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, kesho anatarajiwa kukabidhiwa taarifa za kamati mbili zilizoundwa na Bunge katika Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 kuhusu na makinikia ya almasi na biashara ya madini ya tanzanite. Kwa mujibu wa taarifa za bunge hafla fupi ya makabidhiano hayo itafanyika katika viwanja vya bunge na viongozi wa kitaifa watakuwepo. Kabla ya Waziri Mkuu kukabidhiwa taarifa hizo, kamati hizo mbili zitakabidhi taarifa zake kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai ambaye naye atakabidhi kwa Waziri Mkuu. Taarifa hizo mbili zinazosubiriwa kwa makini hasa baada ya taarifa za kamati zilizoundwa na Rais John Magufuli kuibua makubwa katika makinikia kwenye makontena bandarini. Kamati hizo maalumu zote zilikuwa na idadi sawa ya wabunge ambao ni tisa na zililenga kushauri juu ya mfumo bora wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa biashara ya madini ya almasi na Tanzanite hapa nchini. Kamati iliyohusu almasi ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu

HAMISA MOBETO KUZAA NA BWANAKE… ZARI THE BOSS LADY ATINGA BONGO KUPATA UKWELI

Image
                      Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ . BAADA ya maneno mengi kusemwa Bongo kufuatia madai ya bwana’ke kuzaa na mwanamitindo mwenye jina kubwa, Hamisa Hassan Mobetto, mwanamama mjasiriamali mwenye jina kubwa Afrika Mashariki, Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuendelea kuliamsha dude baada ya kutinga Bongo na kuanza kudodosa ili kupata ukweli wa ishu hiyo. Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho ni makini, awali Zari alitinga Bongo mapema wiki iliyopita na kupigwa chabo na ‘wadakuz’ AKIWA KATakiwa nyumbani kwa jamaa huyo ambaye ni msanii wa Bongo Fleva huko Madale jijini Dar. Akiwa katika pozi. Ilidaiwa kwamba, hata hivyo, hakukaa sana kwani aliondoka kwenda kwenye kumbukumbu ya siku 40 za kifo cha mama yake, Halima Hassan nchini Uganda kabla ya kurejea Bongo wikiendi iliyopita.             Kwa taarifa yenu Zari amejaa tele Bongo na lengo lake ni kuchimba na kupata ukweli juu ya madai ya Hamisa kuzaa na bwana’ke.Unajua akiwa

Polisi wamkamata Mtekaji Watoto

Image
POLISI mkoani Geita kwa kushirikiana na wenzao wa Mkoa wa Arusha wamemtia mbaroni mtuhumiwa wa utekaji watoto akiwa na mtoto mwenye umri wa miaka miwili katika nyumba ya kulala wageni ya Shitungulu, Katoro Wilaya na Mkoa Geita aliyekuwa akimshikilia akidai apewe Sh milioni nne. Samson Peter amekamatwa usiku wa kuamkia jana baada ya timu maalumu ya Polisi ya askari tisa, watano kutoka Arusha wakiongozwa na Mkaguzi wa Polisi Amani na wa Geita askari wanne wakiongozwa na Mkaguzi wa Polisi, James, kuizingira nyumba ya wageni aliyokuwa amejificha mtuhumiwa na mtoto aliyemteka tangu Septemba Mosi. Akithibitisha hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo alisema mtuhumiwa alikamatwa saa mbili usiku juzi katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Shitungulu katika Mtaa wa California, Kata ya Katoro wilayani Geita akiwa chumba namba 11 na mtoto huyo Justine Ombeni (2) aliyemteka, akiwa hai na afya njema. Kamanda Mwabulambo alisema mtoto huyo alitekwa Sept

Mbunge Mteule Viti Maalum CUF, Bi Hindu Mwenda Azikwa

Image
Mwili wa marehemu Mbunge Mteule Viti Maalum Cuf, Hindu Mwenda, aliyefariki nyumbani kwake Kibada Kigamboni ukiwasili makaburi ya Kisutu Dar leo. Maziko yakiendelea. Sheikh (kulia) akifanya  maombi baada mazishi. Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (katikati) akiwa katika mazishi hayo. …Akiongea  na wanahabari baada ya maziko. HATIMAYE Mbunge Mteule Viti Maalum Cuf, Hindu Mwenda ,  aliyefariki usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake Kibada Kigamboni amezikwa leo makaburi ya Kisutu Dar na mamia ya wafuasi wa chama chake na wananchi wengine wa Dar es Salaam. Sheikh aliyeongoza mazishi hayo aliwahimiza wanachama wa Cuf kuendeleza upendo na kufanya kazi kwa ushirikiano ambapo miongoni mwao ni mwenyekiti wa chama hicho anayetembuliwa na Msajili wa Vyama, Profesa Ibrahim Lipumba. Lipumba alimsifia marehemu akisema alikuwa anajituma katika kazi zake na alikuwa mwanachama shupavu na alikuwa mfano kwa wanachama wengine wanaokipenda cha

Uhuru Kenyatta Ampa Onyo Raila Odinga

Image
Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta. Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta a mefunguka na kutoa onyo kwa mpinzani wake Raila Odinga kuwa asahu kuhusu tume mpya ya uchaguzi lakini pia amemtaka Jaji Mkuu wa Kenya David Maraga kutoingilia kwani wao wameheshimu maamuzi ya mahakama. Uhuru Kenyatta mpinzani wake Raila Odinga (kushoto). Uhuru Kenyatta amesema chama chake cha Jubilee kipo tayari kwa uchaguzi huo wa marudio na sasa wanasubiri Tume ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC iweze kutangaza siku ya uchaguzi na wanaiomba itangaze siku hiyo haraka. Aidha Uhuru Kenyatta amesema kuwa wapinzani hao hawana haja ya uchaguzi bali ni watu ambao wanataka serikali ya mseto kitu ambacho yeye hawezi kukiruhusu hata kidogo Mahakama ya juu nchini Kenya Septemba 1, 2017 ilifuta matokeo ya Urais nchini Kenya na kuamuru kuwa uchaguzi mpya ufanyike katika nafasi ya Urais kutokana na mahakama hiyo kubaini baadhi ya mapungufu wakati wa utoaji wa matokeo hayo ya uchaguz

Waziri Mkuu Majaliwa atoa suluhisho la ajira

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watendaji katika mikoa yote nchini kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya viwanda katika maeneo yao kwani  vitasaidia katika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira hususani kwa vijana. Waziri Mkuu alipozungumza na watendaji na wananchi wa mkoa wa Morogoro amesema mpango wa Serikali wa kujenga uchumi wa viwanda ambao unalenga kuinua uchumi wa Taifa kutoka wa chini kwenda uchumi wa kati, hivyo ni muhimu kuvifuatilia. “Viwanda hivi vinatupa uhakika wa ajira nchini kwa vijana kwa sababu vinauwezo wa kuajiri watu wengi na wa kada mbalimbali, hivyo ni muhimu tukafuatilia utendaji wake. Lakini mbali na kutoa ajira nyingi, pia viwanda vitawezesha wakulima kupata soko la uhakika la mazao yao na kukifanya kilimo kuwa na tija," Mhe. Majaliwa. Pamoja na hayo Majaliwa ameongeza na kusema kwamba muda mrefu sekta ya viwanda nchini ilikuwa haifanyi vizuri jambo ambalo lilisababisha kuongezeka kwa tatizo la ajira na mazao yalikosa soko. Ha