Posts

Showing posts from April, 2016

BREAKING NEWZZZZ…JAMBAZI SUGU LAKAMATWA POSTA ,WAWILI WAKIMBIA..NOAH YAKAMATWA

Image
MTU MMOJA ANAYE SAKIKIKA KUWA JAMBAZI AMEKAMATWA JIJINI DAR MAENEO YA POSTA BAADA YA KUTAKA KUMTAPELI MAMA MMOJA ANAYE FANYA KAZI YA TIGO PESA …MASHAHIDI WALIO KUWEPO ENEO HILO WANASEMA HUYO KIJANA ALIFIKA KWA DADA HUYO KWA LENGO LA KUTAKA KUWEPA PESA KIASI CHA TSH.ELFU TANO ..WAKATI YULE DADA ALIKUWA ANAHESABU PESA ZAKE KWANZA NDIPO HUYO JAMBAZI AKAKWAPUA NA KUKIMBILIA NDANI YA GARI AINA YA NOAH..NA KUMRUSHIA MTU ALIYEKUWA NYUMA YA HILO GARI….WAKATI HUO MCHEZO UKIENDELEA NDIPO DEREVA AKAWA ANAJIANDAA KUWASHA GARI NA KUONDOKA NDIPO RAIA WAKAMDAKA DEREVA NA KUMTOA KWENYE GARI …LAKINI DEREVA NA YULE ALIYEPOKEA PESA AKACHOROPOKA ..ILA YULE ALIYEIBA AKANASWA NDO HUYO KWENYE PICHA

Edward Lowassa na Mh.Sumaye kutua kwa kishindo Dodoma leo, bunge lahaha

Image
Aliyekuwa mgombea wa urais wa UKAWA Mh. Edward Lowasa na mwanamkakati wake waziri mkuu mstaafu Mh. Sumaye, wanatarajiwa kutua Dodoma leo kwa shughuli maalum ya kisiasa Taarifa za awali zinasema watakutana na wabunge wa UKAWA kimkakati. Tetesi zinasema kuwa Lowasa ataweka wazi “facts” kwa umma, kina nani wanahusika na kwa nini Bunge halionyeshwi live na kuwataka wananchi kuchukua hatua. Ikumbukwe pia kuwa juzi kati CAG alitoa repoti yake na kuonyesha madudu ya serikali chini ya CCM huku akizivua nguo tawala ya awamu ya nne na awamu ya tano kwa kushindwa kusimamia matumizi ya rasilimali.

Naibu Spika Achafua Hali ya Hewa Bungeni Baada ya Kumwita Mbunge BWEGE.

Image
Naibu Spika Tulia Ackson, ambaye katika vikao vya Bunge anatakiwa kusimamia mijadala kwenye chombo hicho cha kutunga sheria, jana alizua kizaazaa baada ya kumuelezea mbunge wa Kilwa Kusini (CUF), Selemani Said Bungara kuwa ni bwege, akimtaka aache kuonyesha hali hiyo. Kwa mujibu wa toleo la pili la Kamusi ya Kiswahili Sanifu (Oxford) la mwaka 2004, neno bwege linamaanisha “mtu mjinga, mpumbavu, bozi, fala gulagula”. Kitendo cha kutumia neno bwege kumuelezea mbunge huyo kilisababisha wapinzani wacharuke, na kuibua bungeni kesi ya mtu aliyefunguliwa mashtaka mkoani Arusha kwa kosa la kumuelezea Rais John Magufuli kuwa ni bwege. Bila ya kuruhusiwa, mmoja alifungua kipaza sauti na kusema:  “Hatimaye msamiati wa bwege watua bungeni sasa kutumika rasmi. Futa lugha ya kuudhi; bwege bwege.” Hata hivyo, wabunge hao wa upinzani hawakushinikiza Dk Tulia kufuta kauliz yake, lakini baadaye wakiwa nje ya ukumbi waliponda kitendo hicho cha kiongozi huyo wa Bunge ambaye aligombea u

ZITTO KABWE : WAHUSIKA WA SAKATA LA TEGETA ESCROW WABURUZWA MAHAKAMANI.

Image
MBUNGE wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT – Wazalendo) ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kuwafikisha mahakamani wahusika wa sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow ili sheria ichukue mkondo wake. Zitto aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana wakati akichangia kwenye hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, iliyowasilishwa na Waziri Angela Kairuki pamoja na ile ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), iliyowasilishwa na Waziri wake, George Simbachawene. Alisema mwaka 2014, Takukuru waliijulisha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwamba ilikuwa inachunguza na kumaliza uchunguzi kuhusu miamala ya kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenda Benki ya Stanbic Tanzania. Alisema katika taarifa zote ambazo Takukuru inatoa kuhusu kesi za ufisadi, hakuna mahali inapozungumzia maendeleo ya suala hilo. “Hata siku moja hakuna mahala Takukuru wanasema kuhusu uchunguzi huu na lini wahus

Wabunge MABUBU Kubanwa Bungeni......Ni Wale Wanaoshiriki Vikao vya Bunge Lakini Hawachangii Chochote

Image
Kiti cha Spika wa Bunge kimesema ipo haja ya kufanya marekebisho ya Sheria pamoja na Kanuni ili kila mbunge apate posho kulingana na kazi aliyofanya bungeni, badala ya utaratibu wa sasa wa kuangalia mahudhurio pekee. Aidha, kimewataka wabunge kubadilika na kuacha tabia ya kuchukua posho za vikao vya Bunge bila kuzitolea jasho. Kauli hiyo imekuja kutokana na Mwongozo ulioombwa Aprili 25, mwaka huu na Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) ambaye alikitaka kiti cha Spika kutoa Mwongozo kuhusu usahihi wa wabunge wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kulipwa posho na mishahara wakati hawashiriki na kutimiza wajibu wao wa kuchangia kwenye mjadala wa Bunge la Bajeti linaloendelea katika Mkutano wa Tatu wa Bunge la 11. Bashe alisema mbunge huyo alitumia Kanuni ya 68(7) ya Kanuni za Kudumu za Bunge akiomba Mwongozo wa Spika kutokana na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, kuamua kutoshiriki mjadala unaoendelea bungeni, lakini wabunge hao wanasaini na kulipwa mishahara na posho. Hi

Breaking Newzzz…..Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), Bi. Juliet Kairuki

Image

KAJALA AMWANGUKIA RAIS MAGUFULI,AFUNGUKA MAZITO KUHUSU MUMEWE

Image
  Kajala Masanja ‘Kay’ Dar es Salaam: Mtoto mzuri anayebamba kwenye Bongo Movies, Kajala Masanja ‘Kay’ amemuangukia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli ‘JPM’ kuwa kama ikitokea akatoa msamaha wa wafungwa, amkumbuke mumewe, Faraji Agustino ambaye yupo gerezani Segerea jijini Dar akitumikia kifungo cha miaka saba. Akizungumza na Amani hivi karibuni, Kajala alisema kuwa amekuwa akimuwaza mumewe huyo na suluhisho kuu kwa sasa litakalomfanya Faraji atoke gerezani ni msamaha wa rais pekee. “Najua Mungu yupo na atatenda miujiza, namuomba sana Rais Magufuli siku akitoa msamaha kwa wafungwa amkumbuke na mume wangu Faraji,” alisema Kay. Hata hivyo, mmoja wa wanasheria maarufu Dar aliliambia gazeti hili kuwa kosa alilopatikana nalo mume wa Kay huwa halina msamaha wa rais. Machi 2013, Faraji alihukumiwa kifungo cha miaka saba jela au faini ya za zaidi ya Sh. milioni 200 baada ya kupatikana na hatia ya kutakatisha fedha haramu kwenye Benki ya NBC, Taw

UKAWA Wawakaanga Ridhwan Kikwete na Mama Salma

Image
HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam imewakaanga wanaotajwa kumiliki Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) bila kufuata utaratibu,   anaandika Pendo Omary. Hatua hiyo imekuja baada ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inayoongozwa Ukawa kuzuia Sh. 5 bilioni, fedha mali ya Kampuni ya Simon Group Limited. Mama Salma Kikwete, Mke wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete na Ridhwan Kikwete, mtoto wa rais huyo na Prof. Juma Kapuya, aliyekuwa Mbunge wa Urambo Magharibi wanatajwa kuwa miongoni mwa wana hisa kwenye shirika hilo. Simon Group Limited ililipa fedha hizo kwa halmashauri hiyo ikiwa ni sehemu ya malipo ya ununuzi wa hisa za UDA. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Saed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo amesema halmashauri haikuuza UDA licha ya Simon Group Limited kudai kununua. Kwenye mkutano huo ambao pia uliohudhuriwa naIsaya Mwita Charles, Meya wa Jiji la Dar es Salaam Kubenea amesema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 28.04.2016

Image
                     

MAGAZETI YA UDAKU LEO

Image
 

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

Image
     

Wanamuziki, wadau kukutana na Makonda

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda. WANAMUZIKI wa dansi, taarab, Bongo Fleva na wadau wa muziki waishio Dar es Salaam, Alhamisi hii watakutana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda, ili kubadilishana mawazo juu mwenendo wa kazi zao. Mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa Vijana Social Hall Kinondoni kuanzia saa tano ili kujadili changamoto za Sheria ya Biashara ya Vileo na Burudani ambayo iko tangu mwaka 1968 na 1972. Mmoja wa wasemaji wa umoja huo, Juma Mbizo, ameuambia mtandao huu kuwa maombi yao ya kumwalika Makonda yameshawasilishwa kwake. Mbizo amesema mkutano huo hauhusiani na chama chochote cha muziki, bali umeandaliwa na waathirika wakuu wa sheria hiyo.

BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU YAPITISHWA NA BUNGE MJINI DODOMA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihitimisha  hoja  ya makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa fedha 2016/2017 bungeni mjini Dodoma Aprili 27, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera, Bunge ,Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama  akijibu baadhi ya hoja za  kuhitimisha makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa fedha 2016/2017 bungeni mjini Dodoma Aprili 27, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera, Bunge ,Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama  akijibu baadhi ya hoja za  kuhitimisha makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa fedha 2016/2017 bungeni mjini Dodoma Aprili 27, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akipongezwa na wabungeu)baada ya  bunge kukubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 bungeni mjini Do

Maria Nyerere atembelea daraja la Kigamboni

Image
  Mama Maria Nyerere, Mjane wa Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akiwa na mwanae Mhe. Makongoro Nyerere na msaidizi wake akifurahia mandhari wakati walipotembelea Daraja la Nyerere Kigamboni jijini Dar es salaam leo. Mama Maria, ambae hakujali mvua kubwa iliyokuwa inanyesha, alionekana mwenye furaha kufika darajani hapo kwani ndoto ya miaka mingi iliyoanzishwa na hayati mumewe imetimia. Pia alimshukuru sana Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwa kuagiza daraja lipewe jina la Mwalimu na siyo yeye, jambo ambalo amesema limemfariji sana kwani vizazi vya sasa na vijavyo vitamkumbuka mwasisi wa Taifa.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 27.04.2016

Image